MWAKA WA KI-ROHO KWA WALEI
Kwa nini kwanzisha
mwaka wa ki-roho?
Wakati
wa karne ya 20 Mungu alitujalia neema nyingi. Mojawapo ndiyo Upyaisho wa Roho
Mtakatifu. Mwaka 1967, miaka miwili tu baada ya Mtaguso wa Vatican II, kikundi
cha Wakatoliki, huko Marekani, walionja
‘Ubatizo wa Roho Mtakatifu’, yaani nguvu na karama zake. Tangu siku ile
mamilioni wa Wakatoliki walijazwa Roho Mtakatifu, kuongozwa naye, kuwezeshwa
naye kueneza Habari Njema ya Yesu Kristo na kuishi Injili kwa furaha. Baadhi
yao vijana wengi wamejitoa, kwa moyo wote, kufanya kazi ya utume.
Lakini
baada ya miaka kadhaa, wengi wanaanza kukata tamaa wanapokutana na majaribio,
matatizo, n.k., hasa wakionja ukame wa ki-roho. Wanafikiri kwamba Mungu
amewaacha. Basi wanaacha kazi ya utume. Wengine wanajaribu bahati yao kwa
kujiunga na makanisa mengine ya ki-pentekoste. Wengine wanaacha hata kuishi
maisha yao ya kikristo wakisema moyoni: "Nimedanganywa".
Mimi
binafasi nafikiri kwamba kuna sababu nyingine. Shina la matatizo ni kukosa misingi wa maisha ya ki-roho. Mkristo hawezi
kuwa mtume wa kudumu bila kuimarishwa ki-roho. Imani yake isibaki kichwani kama
elimu bali iongoze matendo yote ya maisha yake. Tena imani
isitegemee hisia zake, bali hisia zake zitawaliwe na imani yake. Wengi baadhi
ya vijana waliojitoa kwa Mungu wanabaki katika mang’amuzi ya ‘Ubatizo wa Roho
Mtakatifu’ na hawaendi mbele katika safari zao za ki-roho. Ni muhimu sana
kukutana na Yesu Mfufuka na kwa namna nyingine ni lazima, lakini ‘experience’ hiyo ni mwanzo wa safari ya
Mkristo.
kuhubiri hadharani na kuwaombea watu. Paulo, baada ya ubatizo wake, alienda katika nchi ya Arabuni kwa miaka mitatu, kabla ya kutangaza huko Dameski, kwa muda mfupi, kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu. Na baadaye alikaa Tarso miaka mingi kabla ya kutumwa na Roho Mtakatifu kutangaza Habari Njema ya Yesu kwa Wapagani wote, (Gal 1:15-24). Mungu anahitaji muda kumtayarisha mtu awe chombo kiteule mikononi mwake.
Kutokana
na maelezo hayo hapo juu, ndiyo maana tumeanza Mwaka wa ki-roho kwa walei.
Mafundisho yanalenga waliomtolea Yesu
maisha yao lakini bado wana kiu ya kujiendeleza ki-roho.
Makusudi
ya Kituo hiki ni kujenga misingi ya maisha yao ya ki-roho, kwa njia ya kazi,
sala na mafundisho, na nidhamu ya maisha ya kawaida. Kinawakaribisha hasa Vijana,
wavulana kwa wasichana,- hata watu wazima - wanaotaka kujifunza zaidi, kwa muda
wa mwaka mmoja, misingi ya maisha ya ki-roho, kukua katika imani yao ya
ki-katoliki, kujijengea nidhamu kwa maisha ya mbele na kudumu katika huduma
zao.
Licha
ya sala na mafundisho wanafunzi wanajizoesha kwa njia mbalimbali, kama kwa
mfano, kazi ya mikono, kutafakari porini uumbaji wa Mungu, matembezi kwa miguu
(Tazama: Walking in the footsteps of the
missionaries of the first caravan, 1878-1879), na kufurahi pamoja.
Idadi ya wanafunzi
Kituo
hiki ni kichanga. Kila mwaka, mwezi wa Julai, tunawapokea wanafunzi wapya.
Mwaka 2009-2010 tulipokea wanafunzi 10. Mwaka 2010-2011 wanafunzi 7. Mwaka
2011-2012 wanafunzi 12, kwa Mwaka 2012-2013 tulipokea pia wanafunzi 12. Kwa
mwaka huu 2019-2020 tumepokea wanafunzi 21.
Hakuna malipo.
Ombi
la kujiunga na Shule
Kujiandikisha
Yeyote
anayetaka kujiunga afadhali ajaze fomu, iliyochapisha chini na aitume kwa anwani
iliyoandikwa katika fomu hiyo.
Anayestahili kujiunga na Shule
Makusudi ya Kituo cha Kungwe ni kujenga misingi ya maisha
ya ki-roho ya Wakristo, kwa njia ya kazi, sala, mafundisho na nidhamu ya
maisha. Kituo hiki kinalenga Wakarismatiki
tu waliomaliza semina ya maisha ya ki-roho na semina ya makuzi, waliomtolea Yesu maisha yao lakini, bado
wana kiu ya kujiendeleza ki-roho. Kinawakaribisha hasa Vijana, wavulana kwa
wasichana (umri si chini ya miaka 21), - hata watu wazima (umri isiyozidi 50) -
wanaotaka kujifunza zaidi, kwa muda wa mwaka mmoja, misingi ya maisha ya ki-roho,
kukua katika imani yao ya ki-katoliki, kujijengea nidhamu kwa maisha ya mbele
na kudumu katika huduma zao.Kituo hiki ni kichanga. Tunaweza kupokea watu 18 hadi 20 tu, wanaume 12 na akina dada 8.
Ukubali masharti ya kujiunga na Shule
Hakuna malipo. Hutalipa ada, wala hutalipwa, bali
utafanya kazi asubuhi kutimiza amri ya Mungu: "Kwa jasho la uso wako utakula chakula", Mwa 3:19. Mchana
utafundishwa, utapata nafasi ya kusoma Neno la Mungu na kukaa kimya mbele ya
Mungu Baba: "Ingia katika chumba
chako cha ndani na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye
sirini", Mt 6 :6. Kila mwezi utaweza kwenda jangwani kukaa peke
yake mbele ya Mungu kati ya viumbe na kumsikiliza.Tunaomba T.shs 100.000/- ziwe akiba yako kwa ajili ya matibabu. Kama una bima fika na bima yako, lakini fedha itahitajika bado kwa ajili ya usafiri.
No comments:
Post a Comment